6/21/2004

Hakuna uhusiano kati ya Iraki na Osama!

Tume ya kitaifa inayochunguza tukio la kigaida la Septemba 11, 2001, imesema kuwa hakuna ushahidi kuwa Saddam Hussein alihusika na shambulio hilo. Wamesema kuwa Osama alikuwa na uhusiano wa karibu na nchi za Pakistani (ambayo ni rafiki mkuu wa Marekani), Iran, na Saudi Arabia. Kumbuka kuwa Wamarekani waliambiwa, na wengi waliamini, kuwa Iraki lazima ivamiwe maana ilihusika na shambulio la jengo la World Trade Center. Ushahidi hakuna! Bush na makamu wake Cheney hawajui wajifiche wapi. Kila hoja waliyoitoa inapanguliwa. Habari zaidi soma ukurasa huu.

1 Maoni Yako:

At 6/27/2004 02:51:00 PM, Anonymous Anonymous said...

Marekani ni ubabe tu haina hoja

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com