6/15/2004

vyakula vya kisasa

Rafiki yangu Dan anasema kuwa alipotembelea Tanzania alijisikia vibaya sana. Kwanini? Alikuta kuwa watu wanadhani kuwa kuacha kula vyakula vya asili na kula vyakula vya papo kwa hapo (fast food) kama McDonalds ni moja ya alama ya maendeleo.

Matatizo ya afya yanayotokana na kula vyakula vyenye kemikali na homoni hapa Marekani yanaongezeka kila siku. Watoto wadogo wanakuwa na miili isiyoendana na umri wao. Karibu kila mtu unayekutana naye ana matatizo ya unene kupita kiasi.

Ameniuliza, hivi mfumo wenu wa elimu hauwafundishi watu wenu kuwa vyakula vyenu vya asili ni bora?

Masikini! Angejua. Mfumo wa elimu wa Tanzania???!!!! Sikuweza kumjibu maana nilikuwa nina njaa. Na kuongea juu ya "mfumo" wa elimu Tanzania inabidi uwe umeshiba.

Bob Marley ana wimbo mmoja anasema: Usikubali wakupumbaze wala wakufundishe, sisi tuna akili zetu wenyewe.
Ameimba maneno haya katika Coming From the Cold.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com