6/13/2004

Wimbo wa Ukombozi

Kuanzia sasa nitakuwa nazungumzia suala la ukombozi wa akili kwa nguvu zaidi. Ndio maana nimeanzisha huu ukurasa. Kwanza kabisa napenda ujue kuwa ninaamini kuwa mapinduzi ya zana mpya za mawasiliano ni mapinduzi ya kijamii, kisiasa, kiakili, na kitamaduni. Ili kuhakikisha kuwa mapinduzi haya yanakuwa na faida kwetu Watanzania. Waafrika. Lazima tuhakikishe kuwa tunaimba wimbo wa ukombozi.

Bob Marley ana wimbo unaitwa Redemption Song. Ndiko nimetoa maneno haya: wimbo wa ukombozi. Katika wimbo huo Bob analia kwa hisia, "Hautasaidia kuimba wimbo huu wa ukombozi?" Kisha anasema
"Jikomboe kutoka kwenye utumwa wa kimawazo, hakuna zaidi ya sisi wenyewe atakayeweza kukomboa akili zetu."

Kwahiyo ukija kwenye ukurasa lazima uwe tayari kukubali kufumbua macho. Kutumia uwezo uliopewa na muumba wako kufikiri na kuhoji. Hoji mamlaka. Hoji kila kitu. Jihoji hata wewe mwenyewe. Hoji. Hoji. Hoji.

****************************************************************
Da, nimechoka kweli. Saa nane usiku sasa. Lazima nikalale. Hivi nimekula? Nilishasahau. Jamani nina hamu na ugali wa kisamvu cha nazi. Jamani! mate yananitoka.
*****************************************************************

Sijaamua wiki hii nitaandika nini kwenye makala yangu ya gazeti la Mwananchi. Uwe unasoma gazeti la Mwananchi kila Jumapili. Soma makala iitwayo: Gumzo la Wiki.
****************************************************************

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com