7/26/2004

Saddam Hussein ni Mshairi!

Imeelezwa kuwa Saddam Hussein anatumia muda wake jela kuandika mashairi. Moja ya mashairi yake linamhusu dikteta mwenzake aitwaye George Bush. Pia anapenda sana kutengeneza bustani. Taarifa zinasema kuwa anapenda kula mkate wa Kimarekani uitwao Muffins, na biskuti. Kongoli hapa usome habari nzima. Sijui kama unajua kuwa Saddam ni mtunzi pia wa vitabu. Ameshaandika vitabu vitatu: Zabibah and the King, The Fortified Castle and Men and the City, na Be Gone Demons! Vitabu hivi vilichapwa bila jina la mtunzi. Kongoli hapa usome zaidi.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com