8/03/2004

Hivi...

Hivi wanasiasa wasipotudanganya kura tutawapa?
Inaelekea tunapenda sana kuambiwa kuwa tutajengewa barabara, hospitali, shule, n.k. Hata tunapojua kuwa tunadanganywa, bado tunafurahia. Hivi kinachomfanya Mtanzania afurahie kwa kupiga makofi, kuimba mapambio, na kupiga vigelegele anaposhangilia kudanganywa ni kitu gani?

Akija mgombea akasema, "Mkinichagua sitawajengea barabara wala shule wala hospitali. Mara baada ya uchaguzi hamtaniona hata siku moja. Sina fedha za kuzunguka jimbo langu la uchaguzi. Sitaki kuwadanganya. Nitakachofanya ni kuwa mwakilishi wenu bungeni. Basi." Atachaguliwa?

Hivi kura zisingekuwa kula, wagombea wangegombea?

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com