8/14/2004

Kucheka ni Afya

Hivi unakumbuka enzi za "matani" shuleni? Kuna jamaa walikuwa nadhani hawalali, wanakesha wakitunga matani maana wakija shule kila asubuhi wana matani mapya makali makali. Walikuwa wakiogopeka. Nakumbuka kuna jamaa alikuwa akiitwa Prospa. Huyu hakuna mtu alikuwa anawezana naye.

Kuna mtu alinitumia haya matani ya Kikenya miezi kadhaa iliyopita. Yatazame. Unaruhusiwa kucheka. Kucheka ni bure. Na ni afya. Haya soma:

1.Wewe ni m-short mpaka ukikalia kwa pavement miguu ina hang kwa hewa.
2. TV yenu ni ndogo lazima ufunge jicho moja ndio uone picha.
3. We m-black mpaka una-sweat soot.
4. Manzii wako nim-ugly mpaka alikataliwa ku-act horror movie.
5. Nyumba yenu ni ndogo mpaka lazima utoke nje ku-change mind.
6. Kwenu nyinyi ni wengi mpaka kwa haos (house) kuna round-about.
7. Nyanya'ko mjinga mpaka ali-fail blood test.
8. Kwenu nyinyi ni mbumbumbu mpaka kupata driving licence ilibidi mpelekwe boarding school.
9. Wewe ni m-black mpaka mosquito ikitaka kukuuma lazima itumie tochi.
10. Nywele za watoto wenu ni ngumu mpaka mnazitumianga kama steel wool.
11. Ati siku moja ulitembea kiatu ikaisha, ukaendelea kutembea mpaka miguu ikaisha hadi kwa magoti.
12. Mko wengi kwa haos (house) mpaka kuna rush hours na kukinyesha kunakuwa na traffic jam.
13. Wewe ni m-short unatokanga kwa bed na parachute.
14. Wewe ni mrefu mpaka ni wewe huongezea jua makaa.
15. Chali yako ni mkonda alibloiwa na wind mpaka S.Africa na hana passport.
16.Shingo yako ni refu mpaka ukikunywa maziwa inafika kwa tumbo ikiwa mtindi.
17. Wewe ni mweusi ukikanyanga makaa unawacha footprint za black kwa makaa.

1 Maoni Yako:

At 8/14/2004 01:34:00 AM, Anonymous Anonymous said...

wakenya na kiswahili chao jamani

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com