8/17/2004

Mradi wa Maneno ya Kiswahili

Kuna mradi wa kuingiza kiswahili katika teknolojia ya tarakilishi unaoendesha na kampuni ya Microsoft na Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam. Mtu yeyote anaweza kushiriki katika mradi huu kwa kubonyeza hapa.
Najua kwa watu wasiounga mkono kampuni za kibeberu kama Microsoft mradi huu hautawafaa. Kuna watu, kama mimi, ambao tunaegemea zaidi katika programu za tarakilishi zilizo chini ya dhana ya "open source" ambapo programu hizi (tofauti na programu za Microsoft ambazo kanuni [code] zake ni siri na zinamilikiwa na kampuni hii) zinamilikiwa na mtu yeyote. Programu za tarakilishi za "open source" hazilindwi na sheria ya hatimiliki ambayo nia yake ni kutengeneza faida kwa wachache. Dhana ya "open source" au "free source" inabadili kabisa hakimiliki toka kuitwa "copyright" na kuitwa "copyleft." Watu wengine wanasema kuwa ujamaa wa kweli duniani hivi sasa unaonekana katika vuguvugu la "open/free source" (Open/Free Source Movement) ambalo linaichukua dunia kwa kishindo na kutishia Microsoft. Nchi kama Brazil, China, Vietman, n.k. ziko mbioni kuondoa kabisa matumizi ya Microsoft, hasa serikalini, na kuchukua programu za tarakilishi (software) zinazotokana na "open source" (hasa LINUX/GNU).

Kwa taarifa zaidi jinsi ambavyo "open source" inavyosaidia nchi za ulimwengu wa tatu kuondokana na ubeberu mpya kupitia kanuni za programu za tarakilikishi (software codes) bonyeza hapa.

Ukipenda kujua faida za "open source" kwa Afrika (na madhara ya Microsoft) bonyeza hapa.
Ili kujua kwa undani dhana ya "open source" bonyeza hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com