8/26/2004

Mshahara wa "ukombozi" wa Iraki

Vita ya "ukombozi" wa Iraki ina mshahara wake. Kwa akina Joji Kichaka na wenzake, makampuni yao na yale ambayo wana hisa zake, yanapata tenda na faida za mamilioni ya dola. Ila kwa wazazi ambao wanao, wengine wenye umri wa miaka 18!, wanapigana huko Iraki mshahara wake ni msiba. Watoto wa akina Joji Kichaka na genge lake la watu wanaotaka kuunda "dunia mpya" ambayo itatawaliwa na kundi la watu wachache, watoto wao wako vyuo vikuu wakichukua shahada ili waje kuwa watawala kama wazazi wao. Jana jumatano, mzazi mmoja mlalahoi baada ya kuambiwa kuwa mwanaye kafariki huko Najaf, aliingia ndani ya gereji kuchukua kiberiti na petroli kisha akaingia ndani ya gari la wanajeshi waliomtembelea kumpa taarifa za msiba na kutia gari moto akiwemo ndani. Soma habari yake hapa.

1 Maoni Yako:

At 8/26/2004 11:37:00 AM, Anonymous Anonymous said...

Uchungu wa mwana aujua mzazi.

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com