8/07/2004

NGUGI WA THIONG'O

Ngugi wa Thiong'o, yule mwandishi mahiri, mtetezi, na mtunzaji wa utamaduni wa Mwafrika toka nchini Kenya, amerudi nchini kwake baada ya kuishi uhamishoni kwa miaka 22 na kupokelewa kama shujaa. Bonyeza hapa usome habari hizo. Pia unaweza kwenda HAPA.

Ngugi, ambaye zamani alikuwa akiitwa James Ngugi, aliondoka Kenya mwaka 1982. Wakati huo alikuwa ameshatumikia kifungo kutokana na mchezo wake uitwao Ngaaika Ndeenda ambao serikali ya Kenya ilidai kuwa ulikuwa na ujumbe wa kihaini. Akiwa kifungoni aliandika vitabu viwili: Caitaani Mutharabaini (Shetani Msalabani) na Detained: A Writer's Prison Diary. Toka mwaka 1986, baada ya kuandika kitabu kiitwacho Decolonising the Mind, Ngugi aliamua kuwa hataandika tena vitabu vyake kwa kiingereza bali Kiswahili na Kikuyu. Wanaoweza kutafsiri, watafsiri kama ifanywavyo kwa waandishi wa kifaransa, kihindi, kiarabu, n.k. Kitabu chake kipya, Murogi wa Kagogo, kilichoandikwa kwa miaka 7 kwa lugha ya Kikuyu kinatolewa nchini Kenya mwezi huu. Tafsiri yake ya kiingereza iko mbioni kutolewa.

Sijui kama mlioko Dar Es Salaam mliweza kwenda kumsikiliza hivi majuzi alipoongea na umma pale Mlimani. Ambao hawakuwepo wanaweza kupata habari kwa kubonyeza hapa. Changamoto aliyoitoa natamani watu wasingeichukulia kwa mzaha. Ukoloni umetenganisha kichwa na kiwiliwili. Soma habari aliyoyasema pale Mlimani utanielewa. Kisha jiulize ni lini tutaviunganisha?

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com