8/14/2004

Patrick Balisidya

Ni huzuni iliyoje mwanamuziki Patrick Balisidya ametutoka. Tukumbuke kuwa Hukwe Zawose naye aliaga dunia mwaka huu. Wanamuziki hawa wawili walikuwa na kipaji cha ajabu. Ila ni Watanzania wachache ambao ukienda majumbani kwao utakuta wakiwa na miziki ya watu hawa. Inasikitisha kuwa Balisidya amefariki akiwa analalamika bila kusikilizwa na mtu yeyote juu ya kudhulumiwa vyombo vya muziki na serikali ya Tanzania. Historia ya dhuluma hii ni ndefu. Nitaigusia katika makala ninayoandika juu yake na wanamuziki wengine walioaga dunia wakiwa na majonzi ya kutupwa na jamii. Pitia tovuti hii ya BBC upate habari za maziko yake na pia uone mawazo ya baadhi ya watu kama akina Balozi Dola ambao walikuwa wakimfahamu kwa karibu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com