8/09/2004

Umeshacheka leo hii?

Nimetoka hospitali kuwekewa "vibanzi" (hili neno, vibanzi, sina uhakika kama ni la kiswahili au kichagga!) kwenye sehemu ambazo mbavu zilivunjika na kukunjika kwa kucheka baada ya kutembelea tovuti ya Bill Powers (http://powers-mbongo.freeservers.com/) na kukuta vipande hivyo hapo chini. Kwakuwa kucheka ni afya nimeamua nikugawie na wewe kichekp. Ila hakikisha unatunza mbavu zako. Haya soma hapo chini:


1. Ukipiga yowe bila kusimama kwa miaka 8, miezi 7 na siku 6, utazalisha nishati tosha kupika kikombe kimoja cha chai. (sioni sababu ya kujisumbua kufanya> hivyo. Bora kutumia jiko la mchina) .
2. Ukitoa mashuzi bila kusimama kwa muda wa miaka 6 na miezi 9, utazalisha gesi ambayo itatosha kutungeneza nishati kwa ajili ya bomu la atomiki (hapo sibishi! Watanzania tuongeze mazao ya kunde na maharage na tutapewa kura ya veto Umoja wa Mataifa).

3. Inamchukua nguruwe dakika 30 kukamilisha "orgasm" au bao kwa lugha ya kimtaani. (Kuna mtu anataka kuwa> nguruwe?).

4. Binadamu na papa ndiyo wanyama pekee wanaofanya tendo la ngono kwa starehe (kwa nini nguruwe hakuwekwa kwenye hii list?)

5. Mende huweza kuishi siku 9 bila kichwa chake.

6. Simba huweza tendo la ngono zaidi ya mara hamsini (50) kwa siku. (Bado nguruwe nafaidi zaidi!).

7. Tembo ni mnyama pekee asiyeweza kuruka.

8. Jicho la bundi ni kubwa kuliko akili yake.(nimeshakutana na watu ambao wako namna hii)!

9. Mtu akikuudhi, inakuchukua misuli 42 ya uso wako kununa. Inakuchukua misuli minne (4) kumchapa kibao! (uamuzi ni wako).

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com