9/10/2004

Baba Moi na Mzee Ruksa

Ni kitu gani kinafanya watawala wanapoachia madaraka wana wa nchi wanaanza kuwapenda hata kama hawakuwa viongozi wazuri? Ali Hassa Mwinyi, maarufu kwa jina la Mzee Ruksa, wakati akiwa madarakani nchini Tanzania aliandamwa sana kutokana na utumbo uliokuwa umetawala serikali. Hivi sasa hakuna kiongozi anayeshangiliwa kwenye dhifa za kitaifa kama yeye. Kenya nako, Baba Moi ambaye alikuwa madarakani toka mwaka 1978 hadi aliposhindwa mwaka jana, alikuwa akiandamwa kutokana na rushwa na uchafu mwingine mwingi. Hivi sasa kuna watu wanamuota.

1 Maoni Yako:

At 9/07/2005 01:23:00 PM, Anonymous Anonymous said...

Mzee Ruksa hapendwi na kila mtanzania, wanaompenda mzee Ruksa ni wale wanaopata ruzuku kutoka kwake!! Jee unajua ukweli kuhusu familia ya mzee Ruksa? Uliza utaambiwa hasa ukiwa na binti au dada mrembo.

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com