10/30/2004

MCHUANO WA MAJINA!

Nimepata habari hii toka kwenye blogu mpya ya Mtanzania iitwayo Furahia Maisha Yako. Anasema kuwa orodha hii ni ya majina ya walioingia raundi ya pili katika mchuano wa wenye majina yasiyo ya kawaida. Kweli kuna majina hata mimi ninayetetea umuhimu wa kuwa na majina ya asili yamenitoa jasho nene. Orodha hii hapa:
1. Ndugu TAMPERA NGUNAMABWOKO-Muhitimu wa kidato cha sita shule ya sekondari ya wavulana Tabora mwaka 1992.
2. Ndugu GOGOMOKA MISALABA-Muhitimu wa kidato cha sita shule ya sekondari Minaki mwaka 1998.
3. Ndugu ABDALLAH NYUNDO KICHECHE-Mwanafunzi wa kidato cha kwanza shule ya sekondari Minaki mwaka 2002
4. Ndugu MASANINGA SUMAKU POMBOJOLOWE a.k.a PUMBU-Dereva wa mabasi ya Hood
5. Koplo RUBYENEKO MUGANYIZI BYOMBARIRWA-Mpishi mkuu wa kikosi cha 34 cha Jeshi (34 KJ), Mbeya.
6. Ndugu TAKOTAKO WA PUMBUJE a.k.a AKANANA-Muuza miwa na maji baridi maarufu pale magomeni makutano ya barabara za Rashid Kawawa na Morogoro
7. Mheshimiwa NJENGAFIBILI MWAIKUNGILE-Jaji wa mahakama kuu ya Tanzania
8. Mheshimiwa JOHN POMBE MAGUFULI-Waziri wa Ujenzi Tanzania
9.Ndugu TUNTUFYE MWAIKIMBA a.k.a KIMBA-Fundi majiko maarufu Railway Gerezani Dar es Salaam
10. Ndugu BENADETTA TYETYETYE-Muhitimu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, mwaka 2001 fani ya sayansi ya jamii (BA)

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com