10/13/2004

RAIS JOJI KICHAKA ALIFICHA KIDUDE MGONGONI??

Leo mjadala wa tatu na wa mwisho wa wagombea wawili wa Urais, Kichaka (Bush) na Kerry, utafanyika. Toka walipokutana katika kiti moto cha raundi ya kwanza, kumekuwa na habari za kutatanisha juu ya kitu kilichokuwa kimetuna mgongoni mwa Rais Kichaka, ndani ya koti lake la suti. Wachambuzi wa mambo wanasema kuwa alikuwa amewekewa chombo cha kunasa mtandao usiwaya (wifi au wirelesss network) ili apewe majibu na mshauri wake mkuu, Karl Rove. Sikioni alikuwa ameweka kijitu kidogo cha kusikilizia. Moja ya mifano inayotumiwa kujenga hoja ya kuwa alikuwa akinong'onezewa na mshauri wake aseme nini, ni pale alipokuwa akiongea kisha akasema, "Ngoja, niache kwanza nimalize..." wakati ambapo hakuna mtu aliyesema lolote. Kila mtu alikuwa akimsikiliza, sasa alikuwa anamwambia nani asubiri kwanza amalize? Jambo jingine ni matumizi yake ya misamiati na mabomba makali makali ya Kiingereza ambayo sio kawaida yake. Wachambuzi wanazidi kudai kuwa Rais Kichaka alikuwa akitazama chini kimya kama mtu anayemsikiliza mtu mwingine, kisha ananyanyua kichwa na kushusha mapointi makali mno! Watu wanamshauri Kerry katika mjadala wao wa mwisho leo usiku kumpapasa Kichaka kabla ya kufanya lolote lile. Bonyeza hapa uone picha yake na kidude kilichotuna mgongoni mwake.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com