10/06/2004

SILAHA ZA SUMU

Ripoti ya jeshi la Marekani juu ya silaha za sumu nchini Iraki imetolewa. Ripoti hii sio tu inasema kuwa Saddam hakuwa na silaha za sumu, bali hakuwa na mpango wowote wa kuzitengeneza. Unakumbuka baada ya Bush na mabwana wa vita wenziye kugundulika kuwa walitudanganya kuhusu kuwepo kwa silaha hizi, walikuja na kisingizio kipya. Walisema. "Hatukusema kuwa Saddam alikuwa na silaha ila tulisema kuwa alikuwa na programu ya kutengeneza hizo silaha." Ripoti hii inmaonyesha kuwa sio silaha wala programu. Uongo mtupu. Na utawatokea puani.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com