11/26/2004

BLOGU NYINGINE YA KISWAHILI HIYOOOOO...

Napenda kutangaza kuwa ulimwengu wa blogu una rafiki mwingine toka Kenya. Naye kama ilivyo JIKOMBOE anasema titi la mama litamu. Anaandika kwa Kiswahili. Anasema kuwa alipata mshawasha wa kuwa na blogu baada ya kutembelea JIKOMBOE. Haya ni maneno toka katika blogu yake:
"Juzi katika pilka pilka zangu za kuchakura mtandao nilikutana na " blogu " moja ya kaka kutoka tanzania , amabayo kwa kifupi ilinifurahisha sana kiasi cha kwamba nikaamua kuanzisha yangu piaSasa najua wapiga domo watasema kuwa nimeaanza kuiiga lakini kwa sasa nitawaacha waseme kwani wanamuziki wengi tayari washatuambia kuhusu wenzetu ambao huongea sana jioni tu - watalala ."
Blogu yake inaitwa : MAWAZO NA MAWAIDHA. Mtembelee hapa.


0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com