11/17/2004

Joji Kichaka

Jana usiku nilipata wazo. Wazo lenyewe ni kuwa Rais Joji Kichaka ni madungayembe!
Kama haupo Bongo na ulitoka siku nyingi neno hili litakuacha njia panda. Na haliko kwenye kamusi. Kazi kwako.

Halafu kuna watu wameniuliza eti kwanini napenda kumwita huyu Rais mwizi wa kura Joji Kichaka badala ya jina lake hasa. Napenda kumwita hivyo ili hawa jamaa zake wanaofanya kazi katika yale mashirika ya kijasusi yenye majina yanayoanza na "C" na "F" na kuishia na "I" wasinishtukie! Wakinishtukia nitabadili. Naweza kuanza kumwita Madungayembe.

Na yule gaidi namba moja huwa namwita: Jamaa mwenye madevu anayeishi mapangoni akila tende na halua! Ukitajataja jina lake basi jamaa wa hayo mashirika wanaanza kufuatilia barua pepe zako na kila kitu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com