11/26/2004

KONA YA WANABLOGU WAPYA

Nimeweka ukurasa wa wanablogu wapya. Nimeanza na somo la kwanza. Baadhi ya wanablogu na wale wanaotaka kuanza wamekuwa wakiniuliza maswali mbalimbali. Ukurasa wenyewe uko chini ya makala na hadithi za Freddy Macha. Bonyeza palipoandikwa: Somo La Kwanza. Wenye maswali zaidi wanaweza kuniandikia. Naweza nisijibu haraka. Usiwe na wasiwasi, nitakujibu.
Kuna habari njema za wanablogu wa kiswahili wa Tanzania. Yule mwanadada wa Kenya, Ory Okolloh, anayesoma sheria katika chuo kikuu cha Harvard ameziweka blogu mbili mpya za Watanzania, Kona yangu na Furahia Maisha, ndani ya blogu yake ambaye inapendwa na kusomwa na watu wengi.
Mimi nami nimeongeza blogu nilizokuwa nimeweka hapa. Kona niliyoiita: Blogu za Wana Afrika Mashariki nimeibadili na kuiita Blogu za Waafrika. Nimeongeza blogu kadhaa na nitaendelea kuweka nyingine.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com