11/02/2004

MJADALA WA NDEGE YA RAIS

Mjadala kuhusu ununuzi wa ndege ya Rais wa nchi yangu fukara niipendayo ya Tanzania umepamba moto. Soma baadhi ya mawazo ya wenye nchi wenye:

Maoni ya Joe Nambiza Tungaraza:
Ndugu Wananchi,

Kwanza kabisa naunga mkono maoni ya bwana Ndesanjo Macha juu ya usafiri wa mheshimiwa Rais Mkapa, kwamba wajumbe wa baraza la wachawi kutoka makabila mia mbili na hamsini na saba ya Tanzania washirikiane kutengeneza ungo au fisi wa kusafiria vilivyo na mwendo kasi maradufu zaidi ya ndege za kisasa za magharibi. Kwa maoni zaidi tembelea blogu ya Macha : http://jikomboe.blogspot.com

Pili, baada ya masihara ya hapo juu, mjadala huu wa ndege ya rais umeamsha hisia kali miongoni mwetu watanzania hata wengine wengi tulioko ughaibuni tukakiri kuwa asilani hatuwezi kurejea Tanzania ikiwa mfumo wa sasa na serikali hii vitaendelea kutawala!

Wengi wetu tuna hasira kali na nchi yetu iliyotuangusha na kuzidi kutuangusha hadi hivi sasa. Kuanzia masuala ya mishahara ya Walimu; ada za shule; umeme usiotabirika; kufa kwa huduma za halmashauri ya Jiji; kuporomoka kwa huduma za afya ya msingi; utamaduni wa ufujaji na rushwa kwa wafanyakazi na viongozi wa serikali yetu; uwekaji rehani wa mali ya mtanzania katika jina la ubinafsifishaji na soko huria na kadhalika.
Kuwa na hisia kali ni jambo zuri tu kwani nchi yoyote iliyoendelea au mfumo wowote uliowahi kufanya kazi vyema ulijengwa na wale wenye hisia zenye mrengo mkali.

Bwana Abubakar umetoa ushauri mzuri tu kwamba kama tunataka kufanya madiliko basi na tuanze kusaidia au kurejea nyumbani na kutoa mchango wetu moja kwa moja kwani nguvukazi yetu inahitajika. Ikesha Dan umetushauri tugombee udiwani au ukatibu kata , yaani tuwe pale kwenye ‘grass root level’

Pengine muhimu tukumbuke sababu zilizowafanya wengi waishi ughaibuni. Kama mito inavyofuata mikondo basi sisi binadamu pia tunafuata mikondo inayopelekea kwenye matumaini na uwepesi wa maisha. Hakuna mtu anayeweza kusema hii si kweli. Wengi wetu tunaipenda nchi yetu lakini nchi yetu haina vibarua vya kutosha ambavyo vinaweza kumpa kila mmoja wetu ridhaa wakati wakitoa mchango wenye manufaa kwa taifa.
(Self-actualization - being rewarded for a meaningful contribution in a meaningful career..).
A burnt child dreads fire. Hivyo, si rahisi kwa yeyote kurejea nyumbani na kuingia kwenye siasa ili alete mabadiliko bila kuzingatia sababu zilizomtowa huko nyumbani. Pengine ni vizuri kangalia uwezekano wa kusaidia Tanganyika yetu hapo hapo uliko. Kwani bila mkataba maalum, wengi wetu tumechukua kazi ya ustawi wa jamii kutoka serikalini, na kila mara bila ya shaka tumefika Western Union kutuma fedha kwa wadogo zetu au wazazi waliostaafu.

Katika misingi hiyo hiyo naamini kuna uwezekano kuleta tena matumaini ikiwa tutachangia katika elimu na afya kama watu wa magharibi wanavyofanya na WorldVision au Oxfarm lakini katika vyombo vyetu wenyewe Watanganyika. Na wale wanaoweza kuandika na waandike kukosoa na kuelimishana, ikiwa unafundisha vyuoni huku ulaya basi toa muda kidogo kuchangia mada huko vyuoni Tanzania au muda wa likizo yako katika masemina pale mlimani na kadhalika.

Pia la muhimu tusisahau kuwa PROUD kama waafrika hata kama IMF wangesema nini. Kumbuka hakuna mtu mweupe aliyegawanyika kimawazo kuhusu nafasi yake hapa ulimwenguni. They are convinced that they deserve what they have, whatever the costs.

Mwisho, hivi ni kweli? eti nasikia wanataka kununua helikopta mpya ya rais kwani daraja linaloelekea Nachingwea limevunjika hivyo Mkapa akitaka kumtembelea Mama yake anaogopa kupita kwenye matope!

Wasalaam,

Joe Tungaraza


MAONI YA NYANGU R. MEGHJI:
Jamani,
Sidhani kama kuwa maskini kuna maana usile chakula kizuri au kulala pazuri. Kama nikiomba msaada kutoka kwa jirani yangu kwa ajili ya kununua chakula lakini halafu badala yake nikanunua TV, ina maana yule mtu anidai pesa zake au akasirike? Je kama nimepata njia nyingine ya kupata chakula na nikaitumia ile pesa kununua kifaa kingine?
Nafikiri kutusaidia haina maana watusaidie hata kufikiri. Ninaamini uamuzi wa kununua ndege(asset) ulifikia baada ya "vichwa" kukaa na kutafakari. Hata tuliponunua rada inayoweza kutumika na jeshi pia, watu walipiga kelele kwamba hatukuhitaji teknolojia ya kiasi hicho sasa.
Lakini swali linabaki, ni mara ngapi katika maisha yako unanunua ndege au rada? Naamini hata kama ni maskini, unaponunua kitu basi jitahidi kiwe kizuri na kinachodumu. Ndege za Gulfstream zinajulikana kwa "fuel economy" na ubora.
Baadaye tutaulizwa kwa nini unaendesha gari au kuwa mobile wakati asilimiaa 90 ya nchi hawawezi kuwa navyo. Tungenunua basikeli kwa hela za magari tuliyonayo kila mtu Tanzania angeendesha basikeli...
Wasalaam,
Nyangu.Nyangu R. Meghji

MAONI YA ABUBAKAR FARAJI:

Asaalam ALeykum All!
Laila rais alikuwa na ndege ambayo sasa vipuri nvyake havipatikani maana the company who made it are long out of business....but besides that
Tuna watu wengi wana njaa Tanzania, hawana nyimba bora na mambo mengine mengi ...so does this means Rais asitembelee Benz or a decent Car because the money could be better placed else-where....lets be pragmatic and not over-simplify issues....things are far more complex than many critics would have us think....
Its easy to criticise but all of us Tanzanians living abroad especially or even at home have an opportunity to contribute to this debate in many ways but honestly what have we all done in the last year or six months to contribute to our country.....yet we point the fingers of criticism.....lets suggest some solutions we can come together even on this forum put up some suggestions... they may be totally ignored or one or two will be taken onboard...and we will have contributed positively instead of just criticising.....its our country we are criticising so it is our responsibility...

MAONI YA LAILA WAZIRI:
Habari zenu jamani!!?
Maoni yenu nimeyasoma, ni kweli rais anahitaji kuwa na usafiri wake binafsi kama marais wa nchi nyingine waliokuwa nazo. Lakini ununuzi wa pesa za kiasi kikubwa hivyo ulihitaji fikira za kina.Kama habari zilivyo eleza gharama ya ndege ingeweza kutosheleza elimu ya msingi hapo nyumbani lakini ikaonekana kwamba usafiri wa mtu mmoja ni muhimu kuliko elimu ya msingi ya watoto wengi tu hapa nyumbani. Sio lazima hizo pesa zitumike kama hao wafadhili wanavyosema, matumizi ya kuboresha maisha ya watu wengi yangekubalika zaidi kuliko kuboresha safari za rais peke yake.
SWALI: Kabla ya hiyo ndege rais alikuwa anasafiri vipi? Tatizo lilikuwa nini mpkaka kufikia uamuzi huo?
Kama jibu la swali hili ni kuwa rais has to have his own plane that's a no no.....
Nchi ni kama familia na rais ndio baba( The man)
They say " The man's success is not how much money he has made but what kind of family he has brought"
Baba asijiboreshe bila kujali familia.
Laila Waziri

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com