11/25/2004

MWAMKO WA UMMA

Kabla sijaelekea kwenye mazishi ya bata, napenda kuwauliza kama mnafuatilia mwamko wa umma huko Ukraine. Saa moja na dakika nane zilizopita, Mahakama Kuu nchini humo imemzuia anayedaiwa kuiba kura (kama wanavyofanya watawala wa Tanzania) kuchukua madaraka. Soma habari hiyo hapa. Halafu, makala yangu ya wiki hii katika safu la Gumzo ya Wiki, nchini Tanzania inazungumzia juu ya haki na uwezo wa wananchi kuleta mapinduzi. Nitaiweka makala hiyo iitwayo: MIMI NA WEWE TUNA NGUVU KUSHINDA DOLA mara baada ya kutolewa nchini Tanzania. Yanayotokea huko Ukraine ( na yaliyowahi kutokea Jojia, Ufilipino, Indonesia, n.k. ni moja ya vielelezo vya nguvu walizonazo walalanjaa). Ngoja nielekee kwenye bata maana tumbo limeanza kunguruma kwa ubao.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com