12/29/2004

AFYA: KUNYWA MAJI

Kuna rafiki yangu anapenda sana masuala ya afya na uhai. Kanikumbusha kuwa ni vyema nikawa pia najadili mambo hayo hapa bloguni. Hatuwezi kuwa kwenye mapambano dhidi ya utumwa wa fikra, udhalimu, na ufisadi wa watawala wetu bila kuwa watu wenye afya. Leo nitazungumzia maji.
Ninafahamu watu wengi sana ambao hawana tabia ya kunywa maji hadi wasikie kiu. Au wakiwa na kiu watakunywa sumu kali iitwayo soda. Au watakwenda baa kupata "udirinki." Maji ni muhimu sana kwa afya yako. Kwanza kabisa usifikiri kuwa kazi ya maji ni kukata kiu. Ukisikia kiu ujue kuwa mwili wako umeishiwa maji kiasi ambacho umeamua wenyewe kukushtua. Kiu ni njia ya mwili kukwambia, "Rafiki, mbona umenisahau?" Kwa maneno mengine, hutakiwi uwe na kiu hata siku moja. Kunywa maji hata kama huna kiu ili usipate kiu hata siku moja. Kwa siku usikose si chini ya bilauri nane. Ukitaka kujua maji yalivyo muhimu mwilini, fahamu mambo haya:
Asilimia 70 ya mwili ni maji, asilimia 70 ya ubongo ni maji, asilimia 80 ya damu ni maji.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com