12/10/2004

SULEIMANI NA "HEKIMA" ZAKE

Jina la mfalme Suleimani limenijia wakati nikivunjika mbavu nikifikiria jinsi ambavyo watu mtaani kwetu (Tanzania) na kwingine nchini wanavyoazima majina na kushindwa kuyatamka. Jina langu la zamani, Gregory, lilikuwa likitamkwa Kiregori! Nimemkumbuka jamaa mmoja mtaani anaitwa Selemani. Amenikumbusha habari za mfalme Suleimani wa kwenye biblia. Mfalme huyu anadaiwa kuwa alipewa hekima na mungu wa wayahudi, Yehova. Basi nikajiuliza: hivi hekima zake ndio zilimfanya akaamua kuwa na wake 300 na "nyumba ndogo" 700? Kwa ujumla, usije ukafikiri nimekosea, alikuwa na wanawake 1000. Ili uweke picha hii vizuri akilini mwako fanya mahesabu haya. Mwaka mmoja una siku 365. Yeye alikuwa na wanawake 1000!
Suleimani huyo...

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com