12/12/2004

WAGOMBEA URAIS WA MAISHA

Ukiwauliza viongozi wa juu wa vyama vya upinzani Tanzania wana mawazo gani juu ya Marais ambao katika historia wamewahi kujitangaza kuwa Marais wa Maisha (kama akina Bokassa, Banda, n.k.). Viongozi hawa wakiongozwa na Augustine Lyatonga Mrema (mzee wa "nji hii") , kufuatiwa na John Momose Cheyo (Bwana Mapesa), bila kumsahau Maalim Seif Hamad (anayedai kuwa watu wasio na ndevu makazi yao ni jikoni...) na wengine ambao hata ubalozi wa nyumba kumi hawawezi kupata...watakujibu kuwa Urais wa maisha ni udikteta. Urais wa maisha ni kinyume na misingi na kanuni za demokrasia.

Lakini wakati huo huo, viongozi hawa wamekuwa ni "wagombea urais wa maisha."
Sijui kama unaweza kunisaidia kidogo...siwaelewielewi hawa viongozi wa vyama vyetu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com