1/15/2005

MGEUZIE JOJI KICHAKA MGONGO

Januari 20 Joji Dabliyuu Kichaka ataapa kuwa kiongozi wa sirikali iliyoivamia Iraki kwa sababu za uongo. Walituma matineja na mitutu huku wao wakinyemelea nyuma yao na mirija ya kunyonya "kiwese." Kuapishwa kwa Joji Kichaka kutaambatana na maandamano makubwa sehemu mbalimbali hapa Marikani na dunia nzima.
Siku hiyo Joji Kichaka ataapa kuwa Rais wa nchi hii kinyumea na maandiko ya kitabu anachodai anakisoma kila siku kiitwacho Biblia. Inawezekana hajasoma Matayo 5:33-37 maana angekuwa amesoma hapo sijui kama asingeapa kamwe kama mwokozi wake alivyofundisha. Si unajua kuwa Kichaka ameokoka? Eti ni mlokole. Akitembelea Tanzania labda ataenda kwa Kakobe.
Kati ya mbinu zitakazotumika siku hiyo ya tarehe 20 Januari ni kumgeuzia Joji Kichaka mgongo. Mbinu hii itawaruhusu wapinzani wa Kichaka kuweza kupita vizingiti vya polisi kama watu wa kawaida tu kisha baadaye wanafanya vitu vyao. Tembelea hapa. Wanaharakati wengine wamedai kuwa "Kichaka haendi kokote nasi hatuendi kokote." Wako na Joji sambamba. Wanakula naye bakuli moja. Tembelea hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com