1/06/2005

MLANGO WA SITA WA UFAHAMU AU MACHALE!

Hivi majuzi nilikupa taarifa juu ya machale yalivyowacheza wanyama huko Asia kufuatia tetemeko la chini ya ardhi. Wanyama wana uwezo wa juu sana wa kutumia mlango wa sita wa ufahamu. Kama ulipitiwa na habari hizi zisome hapa na hapa. Binadamu nasi tuna uwezo kama huo ila kutokana na maisha ya kileo na "maendeleo" yake tumesahau kabisa jinsi ya kutumia uwezo huo. Tumesahau pia jinsi ya kutazama mwenendo wa wanyama, upepo, tabia za wadudu, n.k. kuweza kutabiri mambo kama mafuriko, tetemeko, ukame, n.k. Lakini kuna makabila ambayo bado hayajachafuliwa na hiki kitu tunachoita "maendeleo." Makabila haya hayajaathirika na utamaduni wa Kimagharibi. Wao bado wako kwenye "maendejana." Kuna makabila kama haya huko Asia ambayo watu wake, pamoja na kuwa wavuvi na kuishi karibu na bahari, hawakuathirika na janga hili maana machale yaliwacheza! Makabila haya yalihamia huko toka Afrika. Jisomee mwenyewe hapa usije ukasema hii ni hadithi.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com