1/01/2005

NDOTO ZA NYUMBANI

Ziggy Marley ana wimbo unaitwa Dreams of Home toka albamu yake ya Conscious Party. Wimbo huu ukiusikiliza ukiwa ughaibuni unajisikia kutafuta ndege umyonyoe mabawa yake, uyavae, kisha uruke kwenda kwa Mama Afrika!

Wakati wa pilikapilika za sikukuu wanayoiita krisimasi, kuna rafiki yangu aliyeko Ughaibuni alikumbuka nyumbani hadi akajisikia kuwa mgonjwa. Hii ni sehemu ya ni maneno yake:

Lakini nenda Mashariki,magharibi nyumbani ni nyumbani.
Kule Rombo kumechangamka watu wa mijini wanamiminika kila dakika. Wakitoke sehemu mbalimbali. Zile mengele* zimefagiliwa, nyumba zimefunguliwa maana sikukuu imefika watoto, wajukuu, wamefika nyumbani. Ni sherehe, ni vyakukaanga tu, hakuna kuchemsha, ni mchele unaliwa, chapati na mburu*. Huku mbege ikiwa pembeni, redio one,KBC, na nyimbo za sikuku ya noeli zikirindima.Ni nani asiyeyajua haya? Tulie tulioko ughaibuni! Ama hakika nyumbani ni nyumbani.

**NB: mburu ni mbuzi kwa kichagga
- mengele ni sehemu ya mbele ya nyumba ambayo kawaida kule uchaggani inapambwa kwa maua.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com