1/10/2005

NINAKUMBUKA...

Ninakumbuka. Na sitakaa nisahau. Hata siku moja. Ni mwaka 2002, pale kwenye jumba la utamaduni la Urusi. Jumamosi jioni. Harusi ya Mrisho mwana wa Mpoto. Ni Mrisho yule wa Parapanda Theatre Lab. Wale wasanii wa "Tangulia Mwalimu," ambao vitu vyao unaweza kuvisoma hapa na hapa. Katika harusi hii ambayo haijapata mwenziye, usanii, na uafrika/utanzania vilipew kipaumbele. Kwa mfano, shampeni ilikuwa ni madafu! Na tafadhali usidhani hii ni porojo. Badala ya kufungua shampeni kama inavyofanywa kwenye harusi za wengi ambapo kizibo cha shampeni huruka hewani na shampeni yenyewe kumwagiwa kiasi huku watu wakishangilia (sijui huwa wanashangilia kitu gani...kizibo kuruka hewani? Ndio nini sasa!), kwenye harusi ya Mrisho dafu lilikatwa na maharusi kunyweshana!
Nitakupasha zaidi mengine yaliyojiri katika harusi hii ya kisanii na kitamaduni.
Hakika, sitakaa nisahau.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com