1/23/2005

RASTAFARI: SEHEMU YA MWISHO

Ninamalizia viporo. Nimeweka sehemu ya mwisho ya mfululizo wa makala juu ya Urasta. Kama hujasoma mbili za mwanzo, zisome kwanza ndipo uisome hii ya mwisho. Nimeiweka katika kona ya makala zangu, mkono wa kuume, chini ya picha yangu. Inaitwa: Mungu wa Marasta anaitwa JAH.

Ninapenda kuwakumbusha wale wote walioko Tanzania ambao wamekuwa wakiniulizia juu ya vitabu vya Urasta kuwa kile kitabu kilichoandikwa na Horace Campbell kiitwacho Rasta and Resistance: From Marcus Garvey to Walter Rodney bado kinapatikana kwenye duka la TPH mtaa wa Samora, jijini DSM.
Pia kwa watakaoweza kukipata, kitabu cha Dr. Dennis Forsythe kiitwacho Rastafari: For the Healing of the Nation ni kizuri mno. Kama unataka kuzama kwa undani kabisa kwenye falsafa na theolojia ya Urasta na elimu-siri ya kiroho ya Waafrika, kitabu hiki kitakufaa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com