1/10/2005

TSUNAMI NA SIASA ZA "MISAADA"

Misaada inayomiminika kwa waliokumbwa na janga la tetemeko la chini ya bahari imeleta sura mpya katika siasa za misaada na pia kuzua mijadala. Kwa mfano, kuna mjadala uliozuka ukidai kuwa nchi za magharibi hazikuonyesha kujali wakati Iran ilipopata janga la tetemeko la ardhi lililoharibu kabisa mji wa kihistoria wa Bam Desemba, 2003. Lakini jambo ambalo mimi binafsi nimekuwa nikilifuatilia kwa karibu ni kitendo cha India kukataa misaada toka nchi yeyote ile. India imeathiriwa kwa kiasi kikubwa na tetemeko hili ambapo zaidi ya wananchi wake 10,000 wamepoteza maisha (nadhani huu msemo,"wamepoteza maisha" sio mzuri sana...tuseme wamehamia kwingine!) Pamoja na India kukataa misaada, nchi hiyo imetoa misaada ya fedha, ndege, helikopta, n.k. kwa nchi nyingine kama Indonesia, Malyasia, n.k. Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Manmohan Singh alimwambia Joji Dabliyuu Kichaka kuwa nchi hiyo haina haja ya misaada na "tukiona tunahitaji misaada tutawaambia." Inaelezwa kuwa ingawa India ni nchi masikini unapotazama kipato cha kila raia, serikali ya nchi hiyo ni tajiri kiasi ambacho hivi karibuni imeshindwa kujua ifanye nini na fedha zake!
Wachambuzi wa siasa za kimataifa wanadai kuwa India imekataa misaada kwasababu za kisiasa. Inataka kuonyesha ulimwengu (nina maana nchi za magharibi) kuwa yenyewe nayo ni nchi yenye uwezo kiuchumi (na kijeshi pia, si unajua kuwa wana nyuklia tayari tayari kurushiana na Pakistani kama ikibidi?!). Mbinu hii ya kuonyesha uwezo wake itawasaidia katika kampeni za kuingia katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Kwanini nisikupe habari hii usome mwenyewe?

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com