1/16/2005

TUKAE KIMYA?

Ukifungua mdomo.Yakatoka maneno dhidi ya chama twawala, utaitwa mpinzani. Utaonekana unashabikia vyama vya upinzani. Ukiwa na domo kubwa watatafuta namna ya kukuonyesha "dawa yako." Utaona cha mtema kuni. Niliwahi kuuliza, "Hivi mtema kuni aliona nini?

Ukifungua mdomo. Yakatoka maneno dhidi ya vyama vya upinzani. Utaonekana msaliti.
"Kanunuliwa siku hizi." Wataanza kunong'onezana. Baadaye sauti itakuwa kubwa. Itakubidi uzibe masikio.
Umenunuliwa. Umesaliti.

Hivi haiwezekani mtu kuwa Mtanzania na kutoa mawazo na maoni yako kama mtu huru bila kuwa mfuasi wa chama "twawala" wala wa upinzani?

Kwanini nisiseme
Huku nina mdomo?
Nisifikiri
Huku nina fikra?
Nisitende
Huku nina haki?
Usinilaumu
Kwa dhuluma
Iliyoivaa nchi
kama kanzu,
Sikuwachagua.

Sijawahi kupiga kura
Toka nizaliwe
Wala sijilaumu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com