1/24/2005

ZILE KUTA ZITAANGUSHWA LINI?

Uhuru wa kutoa mawazo, kufikiri, na kujieleza ni muhimu mno kwa mwanadamu. Hatuwezi kukubali uhuru huu kuchezewa ili kutimiza matakwa ya "watwawala" wachache. Ni kutokana na sababu hii ndio nimeweka kitabu kilichopigwa marufuku na sirikali Tanzania kinachohusu mauaji ya Mwembechai. Kitabu hiki kiko katika kona ya tovuti mchanganyiko, upande wa kuume wa blogu hii. Ingawa sikubaliani na mengi yaliyomo ndani ya kitabu hiki, huyu bwana ana haki ya kujieleza. Kama tutaruhusu tu wale wanaoandika mambo ya kusifia na kufurahisha wakubwa, maana halisi ya uhuru wa habari itakuwa imepondwapondwa.

Sasa kule Kenya ambako tulizoewa kusikia vyombo vya habari vikiimba habari za Moi (mara kenda kanisani, mara kakohoa, mara kanywa maji kijijini kwake...) zile kuta ambazo Ndimara Tegambwage na Horace Kolimba waliwahi kuzizungumzia (kuta zinazozuia maendeleo ya fikra) zinaongezeka urefu. Nimepata habari hii hapa ya mwandishi wa Kenya toka kwa mwanablogu huyu.


0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com