2/28/2005

BLOGU ZA SAUTI ZA HUTBA YA LOUIS FARRAKHAN

Nilijaribu kutuma kwa njia ya simu baadhi ya vipande toka kwenye hutba (uliyenipa neno hili unajijua, uko Texas) ya Louis Farrakhan wa Taifa la Waislamu. Vipande vyenyewe ni vifupi kwa sababu mbili: 1. Unapotuma ujumbe kwenye blogu kwa njia ninayotumia huwezi kutuma kwa muda mrefu.
2. Kwakuwa nilikuwa na Ndesanjo mdogo, Ukweli Macha, ambaye ana miaka miwili na nusu, kuna wakati alikuwa akitaka kuishika simu ili acheze nayo. Ilikuwa ikitokea anaitaka simu inabidi nitume na kuizima simu.

Kuna baadhi ya vipande nimeviondoa maana sauti ya Ukweli ilikuwa inasikika zaidi ya Louis Farrakhan, nami leo sikuwa na nia ya kuwasikilizisha Ukweli bali Farrakhan.

Baadaye nitaandika kwa ufupi aliyoyasema. Hata hivyo, sikiliza vipande vichache nilivyoviweka.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com