2/20/2005

JE MHUBIRI LOUIS FARRAKHAN ANACHUKIA WAYAHUDI?

Nilipotoa tangazo la sikukuu hii inayosherehekewa na Taifa la Waislamu (Nation of Islam) baadhi ya wasomaji walioniandikia wanaongelea jambo ambalo limejaa kwenye vyombo vya habari vikubwa: 1. Farrakhan anachukia wayahudi 2. Taifa la Waislamu wanachukia watu weupe.
Mhubiri Farrakhan sio peke yake anaandamwa kuwa anachukia wayahudi. Mwanazuoni Profesa Tony Martin aliyeandika kitabu cha The Jewish Onslaught naye amekuwa akiandamwa hata kwa vitisho vya kuuawa kwa madai kuwa anachukia wayahudi. Kutokana na wayahudi kushikilia vyombo vikuu vya habari pamoja na makampuni makubwa ya filamu na muziki, mtu yeyote akiongea jambo baya juu yao ataandamwa kila kona kiasi ambacho kila mtu ambaye hafanyi utafiti wa kina ataamini kuwa huyo mtu anachukia wayahudi.
Kama nilivyowahi kusema, watu wengi wanamfahamu mhubiri Farrakha kwa kupitia CNN na mashirika mengine ya habari. Huwezi kumjua Farrakhan kamwe kwa njia hiyo. Msikilize wewe mwenyewe ndipo utoe uamuzi juu yake. Kuamini upande mmoja unakuwa sawa na hakimu ambaye anasikiliza upande wa mashtaka bila kutoa nafasi ya kusikiliza upande unaoshtakiwa. Wewe ni hakimu, umesikiliza upande wa kina CNN na waongo wengine wakisema kuwa Farrakhan anachukia wayahudi. Sasa mpe Farrakhan nafasi ya kujitetea kwa kusikiliza kauli toka mdomoni mwake.
Hivi majuzi nikiongea na rafiki yangu Philin, ambaye kila dakika tunayokutana lazima tuwe na jambo la kubishana, aliniambia kuwa ni kweli kuwa Farrakhan anachukia wayahudi. Nikamwambia kuwa kama Farrakhan anachukia wayahudi kwa kuwasuta na kuwaandama juu ya madhambi na mapungufu yao, basi mtu wa kwanza kabisa kwa chuki dhidi ya wayahudi sio Farrakhan bali ni mwokozi wake (Philin ni mkristo) yeye ambaye ni Yeshua (Yesu Mzanareti). Anachosema Farrakhan leo juu ya wayahudi hajaanza yeye. Yote yalishasemwa tena kwa ukali zaidi zaidi ya miaka 2000 iliyopita na Yeshua (Yesu).
Farrakhan amewahi kupata vitisho mara nyingi vya kuuawa au kupelekwa mahakamani au mbele ya seneti toka kwa wayahudi . Mambo wanayomfanyia Farrakhan walimfanyia hata Yeshua (Yesu). Yeshua alipokuwa akiongea juu ya wayahudi, wayahudi hao walimjia juu kwa kunyanyua mawe ili wampige. Sikiliza kwa makini yanayotoka mdomoni mwa Farrakhan, kisha fuatilia chuki na tuhuma za uongo toka wayahudi na wengine dhidi yake. Kisha rudi nyuma miaka 2000 iliyopita uone yaliyotokea kwa mhubiri mwingine aliyedaiwa kuwa anachukia wayahudi. Ili urudi nyuma wakati huo, soma mwenyewe kitabu cha Injili ya Yohana 8:31-59. Kama huna biblia nenda hapa. Soma vyema mstari wa 59.
Mwenyewe utaniambia.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com