2/20/2005

MAAFA YA NAGASAKI

Mwaka 1945 Marekani iliweka "rekodi" kwa kuwa nchi ya kwanza na pekee hadi leo hii kutumia bomu la atomiki dhidi ya binadamu wasio na hatia yoyote ile. Bomu hili lilitengenezwa kwa madini ya uraniumu toka nchi ya Jamhuri ya "Kidemokrasia" ya Congo. Tazama picha hizi za maafa haya yaliyofanywa na taifa hili linalojipa ukiranja wa kupeleka "demokrasia" nchi nyingine kama Afghanistani, ambako inadaiwa kuwa wanawake wamekombolewa (sijui kwanini hawaendi kukomboa wanawake wa Saudi Arabia ambao hawaruhusiwi kupiga kura, kugombea nafasi za uongozi, kuendesha magari, kupewa visa au pasi ya kusafiria bila kuandamana na mwanaume, n.k.). Bonyeza kwenye neno "next" ili uweze kutazama picha zote.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com