2/11/2005

MAKALA MPYA KUHUSU UTAMADUNI

Kutokana na mwezi huu kuwa ni wa kumbukumbu ya historia ya waafrika wenzetu wa Marekani, nimeandika makala kuhusu utamaduni. Nenda katika kona ya makala zangu uisome. Inaitwa: KAMA UNAPENDA UTAMADUNI, MBONA UNAVAA NGUO?

Napenda pia kuwaomba msamaha wasomaji wangu kwa kuwa sijatimiza ahadi ya kuweka makala za Padri Karugendo ambaye ameshanitumia. Kona yake itakuwa tayari kabla ya mwisho wa wiki. Pia ile kona ya Freddy Macha itakuwa imefanyiwa ukarabati na kuongezewa makala mpya.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com