2/12/2005

NATANGAZA MAMBO MAWILI

Kwanza, ni kweli kuwa kuna watu, kwasababu wanazojua wao na waliowatuma, wamenitaka niache kublogu. Kwani unadhani nilitaka kujua eti kwanini niache kublogu? Huko ni kupoteza muda muhimu. Natatumia muda huo kuzungumza na ukimya. Sina haja ya kujua sababu maana hakuna sababu zozote zinazoweza kunisimamisha kublogu. Napenda kuandika na kuna watu wanapenda kusoma. Nukta! Kituo! Mimi kama raia wa nchi yangu nina haki ya kikatiba ya kutoa maoni na kuyasambaza kwa wengine (ndio, ili wanyanyuke na kuwanyang'anya ulaji). Nina haki hiyo pia kama binadamu.

Pili, jamaa ambaye kisa cha Mswahili na mtoto wa kizungu kinatokana na maisha yake, ameshtukia stori. Anasema kuwa ingawa sijamtaja jina, anajua kuwa nimeandika maisha yake na hataki kusoma mtandaoni. Bado tunabishana juu ya kukiondoa au kukiacha kisa chenyewe ndani ya blogu. Hivi nilifanya kosa? Kisa chenyewe kinasisimua. Na isitoshe sikumtaja jina na mambo mengi nimebadili hata watu wenyewe aliohusika nao wakisoma hawataelewa chochote. Kosa liko wapi?

Ngoja nifikirie.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com