2/27/2005

Nchi ya Liberia ilipata "uhuru" mwaka 1847. Neno "Liberia" linamaanisha "nchi ya watu huru." Mwanzoni nchi hii ilipokaliwa na Wareno iliitwa Pwani ya Nafaka/Punje. Mji mkuu wa Liberia ulipewa jina lake, Monrovia, kutokana na jina la aliyekuwa rais wa Marekani na rais wa chama kilichokuwa kikiendesha kampeni ya kuhamisha waafrika weusi wa Marekani waliokuwa wameachiwa toka katika makucha ya utumwa. Rais huyo aliitwa James Monroe na chama hicho kiliitwa America Colonization Society. Idadi ya wahamiaji wa kwanza, waliojulikana kama Americo-Americans, ilikuwa ni 86. Toka mwaka 1861 hadi 1847, watumwa walioachiwa huru waliohamia Liberia walipata 13,000. Jeshi la majini la Marekani liliongoza juhudi za mikataba ya uhusiano mwema kati ya wahamiaji na wenyeji. Watu wengi hudhani kuwa Waafrika Weusi toka Marekani walipohamia nchi hiyo, hakukuwa na watu. Kulikuwa na wahamiaji walitoka sehemu mbalimbali kama Mali, Ghana, Sudan, n.k. Wahamiaji walijitofautisha na wenyeji kwa kutumia neno "Mr" kwa wanaume, na walishika sehemu zote muhimu za uongozi. Rais wa kwanza wa nchi hiyo, Joseph Jenkins Roberts alizaliwa nchini Marekani. Rais wa kwanza mwenyeji toka makabila ya wenyeji (ambao hawakuhamia toka Marekani) alikuwa ni Sajenti Meja Samuel Doe aliyechukua madaraka kwa nguvu mwaka 1980.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com