2/20/2005

NDESANJO NA TAIFA LA WAISLAMU

Napenda kutoa ufafanuzi kidogo. Mimi sio mfuasi wa Taifa la Waislamu ingawa ninafuatilia kwa karibu sana mambo yao. Ninafanya hivi kwasababu za kitaaluma na sio kidini. Na ninapenda Waafrika wengine wajue kwa undani juu ya vuguvugu hili la waislamu weusi. Kuna mambo anayosema Farrakhan ambayo ninakubaliana naye, ila kuna mambo ambayo sikubaliani naye. Kwa mfano, sikubaliani naye kuwa dini ambayo mungu alimpa mwanadamu baada ya kumuumba ni uislamu. Taifa la Waislamu wanaamini kuwa mungu alipomuumba mwanadamu hakumwacha bila dini. Na dini aliyompa, dini ya kwanza ya mwanadamu, dini ya kweli, dini ya asili ni uislamu. Wakifikia kwenye kipengele hiki mimi huziba masikio!

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com