2/28/2005

NGUVU YA UMMA NDIO HII

Watawala wa nchi fulani za Afrika ambazo sitaki kuzitaja hasa ile yenye jina linaloanzia na T wasije wakadhani kuwa mambo kama yanayotokea Lebanon hivi sasa yanatokea kwa wengine tu. Usicheze na nguvu ya umma. Hoja yangu kubwa siku za hivi karibuni imekuwa ndio hii: wananchi wana nguvu kubwa kushinda nguvu za dola, nguvu za pesa viongozi walizoiba kwa wananchi...wana nguvu kushinda hata hofu ya kifo. Nguvu yao na kauli yao inashinda kitu chochote kile.

Inachukua muda wananchi kujua nguvu waliyonayo, ila wakishajua hakuna kurudi nyuma. Tazama nguvu ya umma huko Lebanon kwa kubonyeza hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com