2/17/2005

NINASOMA THE BAGHDAD BLOG

Leo nimeanza kusoma kitabu kiitwacho Salam Pax: The Baghdad Blog. Kitabu hiki kinatokana na blogu ya kijana mmoja wa Iraki aliyekuwa akitupasha habari za hali halisi nchini Iraki. Alikuwa akiblogu hapa. Kitabu chake kinatarajiwa kuwa filamu.

Katika blogu yake na pia ndani ya kitabu amemnukuu ujumbe huu: "the West won the world not by the superiority of its ideas or values or religion but rather by its superiority in applying organized violence. Westerners often forget this fact, non-Westerners never do, " toka kwa Samuel P. Huntington aliyeandika kitabu ambacho ukikipata usiache kukisoma kiitwacho The Clash of Civilizations and the Remaking of World Order. Katika kitabu hiki, hoja yake kuu ilikuwa ni hii: mgongano mkubwa wa karne hii na zijazo hautakuwa kati ya taifa na taifa au juu ya itikadi au uchumi bali kati ya tamaduni na tamaduni. Kwa undani zaidi soma hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com