2/25/2005

PADRI KARUGENDO AJA NA: UISLAMU NA UKRISTO NDIO TATIZO TANZANIA!

Sasa ndio jua linaanza kuchomoza. Padri Karugendo ana makala mbili nzuri sana katika safu yake iitwayo Kalamu Ya Padri Karugendo (ambayo iko chini ya makala za Freddy Macha, mkono wa kuume wa blogu hii). Ukisoma makala zake hizi utazidi kujua kwanini kanisa lisilopenda mabadiliko, kanisa lisiloambilika la Katoliki la Kirumi haliwataki watu kama Karugendo. Mimi nami nimeingiwa na mori, ninaanda makala juu ya kanisa hili linaloongozwa na wazee wanaojifanya kuwa wanaishi maisha ya useja. Wazee wasio na wake. Moja ya makala yake inaitwa: Kanisa Sasa Liongozwe na Wanawake.
Makala hii ni kinyume kabisa na kanuni za kanisa katoliki zilizotungwa na wanadamu wenye dhambi pengine kushinda hata mimi na wewe.
Makala nyingine ambayo inatisha, hasa ukichukulia kuwa imeandikwa na Padri, inaitwa: Adui wa Tanzania: Uislamu na Ukristo!

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com