2/14/2005

WAGOMBEA ULAJI

Msururu wa wagombea ulaji, wengine wanauita urais, unaendelea kuwa mrefu. Wako wanaotangaza nia yao kichinichini, wako waliotamka hadharani, wako walioanza kuchukua fomu. Katika hawa nasikia Sumaye naye yumo. Sijui anafikiria nini. Hivi hana washauri?
Mwaka 1995 mjini Dodoma, hayati Mwalimu Nyerere alitaja sifa ambazo mgombea urais wa Tanzania anapaswa kuwa nazo. Alisema kuwa mgombea urais lazima aonekane kukerwa na rushwa. Mtu huyo lazima awe tayari kukabiliana na tatizo hilo.
Mwalimu akawaambia wajumbe wa CCM, "Ndugu wajumbe mkiulizwa mgombea huyu ana uwezo wa kupambana na rushwa jibu liwe ndio, litoke ndani ya moyo na si mdomoni...."
Toka mwaka huo 1995 hadi leo hatujapata mtu ambaye ameonekana kuchukia rushwa kwa moyo wake wote na kupambana nayo.
Nikiulizwa kama Sumaye ana uwezo wa kupambana na rushwa (ambayo naye ametuhumiwa mara nyingi kushiriki!) siwezi kusema 'ndiyo' toka moyoni. Sio hivyo tu. Siwezi hata kusema 'ndiyo' toka mdomoni!

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com