4/20/2005

KUMEKUCHA!! BLOGU NILIYOKUWA NIKIISUBIRI IMEKUJA...

Nilipanga kublogu habari hii leo asubuhi lakini kwa kuwa asubuhi la leo lakini kutokana na sababu za kiufundi nilishindwa. Ninadiriki kusema kuwa katika ulimwengu wa blogu za Kiswahili ndio kumekucha sasa. Blogu niliyokuwa niliyokuwa nikiisubiri kwa muda mrefu sana imejitokeza toka matawi ya chini huko Australia. Hii ni blogu iitwayo Mwandani ya Joseph Nambiza Tungaraza, Mtanzania anayeishi nchini Australia. Hivi ndivyo anavyosema mwenyewe juu ya blogu hiyo: Mwandani keshaingia ulimwengu wa blogu.Humu ndani ya blogu hii nitapeperusha mawazo kadiri yanavyovinjari kichwani – siasa, utamaduni, sanaa, mapenzi, ubinadamu, mahusiano ya watu wa rangi tofauti, matabaka tofauti, mataifa tofauti - kadhalika maswala ya haki na demokrasia yetu Waafrika.

Ukienda katika blogu hiyo utakutana na mjadala mfupi kuhusu kifo cha Papa Yohane Paulo. Nimependa sana hoja anazojadili. Nimependa kwa mfano pale anaposema kuwa kama uchaguzi wa Papa ni uchaguzi wa mwakilishi wa Mungu duniani, hakuna haja ya watu kutaka eti Papa atoke sijui Afrika au Marekani ya Kusini. Ninakubaliana naye kabisa maana kwa mungu sisi wote ni familia moja. Hakuna masuala ya rangi au jiografia. Haya, tembelea blogu ya Mwandani (au tuseme mtembelee Tungaraza) hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com