4/11/2005

MAKALA ZA PADRI KARUGENDO HIZOOOOO....

Nimeweka makala tano mpya za Padri Karugendo katika kona yake hapa bloguni iitwayo Kalamu ya Padri Karugendo. Kona yake iko upande wa kuume, chini ya makala zangu na za Freddy Macha. Nitaziweka makala hizo hapa, ila unaweza kuzisoma wakati wowote (hizi mpya na nyingine za nyuma) katika hiyo kona yake. Nimeweka pia makala moja katika kona hiyo, ambayo haijaandikwa na Padri Karugendo. Makala hiyo imeandikwa na ndugu Khalid S. Mtwangi. Yeye alikuwa akijibu makala ya Karugendo isemayo yu wapi Desmond Tutu wa Tanzania. Makala zenyewe ni hizi: 1. Buriani kwa Papa Paulo, hapa. 2.Mangula Ana Maana Gani? Hapa. 3. Nyamwasi wa Chuo Kikuu Dasalama, hapa. 4. Mtoto wa Mkapa na Harusi ya Kifahari, hapa. 5. Vyombo vya Habari, Utamaduni na Mila za Kiafrika, hapa. Makala ya Khalid Mtwangi iko hapa. Makala hii ni jibu kwa makala hii hapa ya Padri Karugendo. Nipatapo nafasi mwezi ujao nitajaribu kujibu baadhi ya hoja alizotoa bwana Mtwangi. Nadhani mjadala huu ni mzuri sana. Unafaa kuendelezwa, kupanuliwa, na kurefushwa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com