4/17/2005

MWANA BLOGU WA KWANZA WA KIKE WA KISWAHILI!!!

Hayawi, hayawi, yamekuwa! Hatimaye mwanablogu mwanamke wa kwanza wa Kiswahili duniani amebisha hodi kwenye ulimwengu wa blogu. Nasi tunaitikia: Karibu mwanamama, binti Afrika!
Kwa muda mrefu nimekuwa nikijiuliza, ni lini atatokea mwanamke mwanablogu toka Tanzania? Sauti ya wanawake toka Tanzania inahitajika kwenye ulimwengu wa blogu kwakuwa sauti hiyo imekandamizwa kwa muda mrefu na kudhihakiwa katika vyombo vikubwa vya habari. Mwanablogu huyo anayeandika historia anaitwa Zainab Yusuph. Anasema: Dunia sio mbaya, walimwengu ndio wana visa! Katika ukurasa wa maelezo yake binafsi anatuambia: Mkombozi wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe. Tembelea blogu yake hapa.
Kwa ujumla hivi sasa kuna blogu kumi za Kiswahili. Kenda toka Tanzania na moja toka Kenya. Ipo nyingine ya kumi na moja ambayo bado mwanablogu mwenyewe hajapenda iwekwe hadharani. Polepole ndio mwendo, walisema wahenga. Ukitaka kutembelea blogu hizo nenda kwenye kona ya viunganishi vya blogu za Kiswahili, upande wa kuume wa blogu hii (chini ya maelezo binafsi na makala mbalimbali).

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com