4/08/2005

NIMEJICHIMBIA

Nimekuwa kimya kidogo. Sababu ya ukimya huu ni kuwa nimejichimbia kwa maandalizi ya mada nitakayoitoa mwezi ujao katika mkutano wa masuala ya teknolojia na watu weusi utakaofanyika katika chuo kikuu cha California, Santa Barbara. Mkutano huo unaitwa Afrogeeks: Global Blackness and the Digital Public Sphere. Mada yangu inahusu blogu zinazotumia lugha za Kiafrika. Kwa wale waliomsoma Ngugi katika "Moving the Centre" na "Decolonising the African Literature," ninajaribu kupanua hoja kuu katika vitabu hivi (na vingine kama hivi). Ninatazama changamoto mpya kwa tamaduni na lugha za Kiafrika katika zama hizi za maarifa/habari, na utandawazi. Habari zaidi za mkutano huo nenda hapa. Mkutano kama huu ulifanyika pia mwaka jana. Tazama hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com