4/25/2005

PAPA ANGETOKEA AFRIKA?

Kabla papa mpya kuchaguliwa na wanadamu (ni wanadamu wanapiga kura kuchagua papa na sio mungu), baadhi ya wasomaji walikuwa wananiuliza kama nilikuwa naunga mkono suala la papa mpya kutokea Afrika. Nilishindwa kuwajibu. Sifahamu kwanini waliniuliza swali namba mbili kabla hawajaniuliza swali namba moja. Wangeniuliza kwanza kama ninaunga mkono kuwepo kwa cheo cha upapa hapa duniani. Au kama ninajali kuwepo kwa cheo hicho. Au kuwepo kwa kanisa katoliki la kirumi kabisa.
Nini kitafanya nijali kuwepo kwa kanisa hili la kirumi lililodanganya watu wangu wakaacha imani zao? Labda siku wakiondoa herufi "R" kwenye RC, yaani Roman Catholic na kuweka herufi "A" ili kuwa na AC, yaani African Catholic. Hebu niache kupoteza muda, kwanza hata hiyo African Catholic ya nini?
Hivi papa angetokea Afrika, angehamia Afrika na kuanza kunywa mvinyo wa asili kama mbege badala ya mvinyo toka magharibi? Kuna rafiki yangu mhubiri ambaye hivi karibuni ataanza kutoa mbege kila jumapili kama damu ya yesu iliyomwagika msalabani kwa dhambi za wanadamu. Ingawa habari yote hii ya damu kumwagika najua ni riwaya fulani, kitendo cha kutumia mbege kinanifanya nitake kuingia kanisa lake. Mchungaji anamhimiza muumini, "Ria se kidogo kwa jina la Bwana!"

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com