5/03/2005

BLOGU NYINGINE YA KISWAHILI YA BINTI WA KITANZANIA

Wahenga walituambia kuwa mwenda pole hajikwai. Ndivyo wafanyavyo wanablogu wa kike wa kiswahili. Wanakuj polepole. Kwanza alijitokeza Zainab. Sasa kajitokeza dadetu Martha na blogu yake nzuri iitwayo "Kutoka Ugogoni." Msome hapa. Karibu Martha Mtangoo.

Ugogoni kwa wale wasiofahamu ni Dodoma, katikati ya Tanzania. Kabila kubwa mkoani hapo ni la Wagogo. Dodoma, kwa mujibu wa sirikali, ndio mji mkuu wa Tanzania. Usinihoji zaidi kuhusu hili. Sidhani hata kama viongozi wenyewe wanaweza kukwambia kwanini Dodoma ndio mji mkuu na sio Dar es Salaam.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com