5/02/2005

CHE GUEVARA ALIKUWA NA JINA LA KISWAHILI

Kumbe Che Guevara na Wakuba waliokuwa msituni kule Congo wakipambana na mabeberu walijifunza Kiswahili maana ilikuwa ndio lugha ya mapambano. Pia walijipa majina ya Kiswahili. Shujaa Che Guevara jina lake la Kiswahili lilikuwa ni Tatu. Nimeipata katika insha ya Mulokozi niliyoigusia muda mfupi uliopita. Unaweza kuisoma mwenyewe hapa. Halafu kama una nafasi/uwezo wa kuiona au kununua filamu kuhusu Che ya The Motorcycle Diaries fanya hivyo. Hutajilaumu. Kuhusu filamu hiyo bonyeza hapa. Na ukitaka kusoma au kusikiliza hotuba zake nenda hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com