5/05/2005

MAONI NA FALSAFA ZA SHUJAA MARCUS GARVEY

Kuna wakati unasoma jambo, linakuingia hasa hadi unaamua kuacha kusoma na kwenda kunywa maji, kujisaidia, kujinyoosha, kutengeneza chai, kisha unarudi tena kusoma. Ndio imenitokea leo nilipotembelea blogu ya Mwandani. Nimekwenda hapo nikakuta amemnukuu shujaa Marcus Mosiah Garvey. Nimechukua nukuu hiyo. Hii hapa:

Ni wachache tu kati yetu, ambao wanaelewa ni kitu gani kinachomfanya mtu awe mtu!Namaanisha -Mtu asiyeweza kufa moyo; mtu asiyeweza kukata tamaa;
Mtu asiyetegemea wengine wamfanyie yale anayoweza kuyafanya yeye mwenyewe;
Mtu asiyemlaumu Mungu, asiyelaumu mazingira;
mtu asiyelaumu ‘bahati mbaya’ kwa hali yake kimaisha;
Bali yule mtu awezaye kutoka na kujitengenezea mazingira yanayomwezesha kuishi.
Kweli nawaambia, ikiwa sisi watu weusi milioni mia nne tungekuwa tunajitambua,
Na tungetambua kwamba ndani yetu tunao uwezo na haki,
Na kwamba tunayo mamlaka kamili,
Ama kwa hakika nawaambieni, mnamo masaa ishirini na nne tu yajayo tungekuwa na taifa jipya,
Tungekuwa na dola iliyosimama kisawasawa,
Si kutokana na matakwa ya watu wengine wowote ya kutaka kutuona tunatengenekewa,
Bali kutokana na moyo wetu dhabiti wa kutakaka kujiinua,bila kujali watu wengine humu duniani wanatufikiriaje.
-Marcus Mosiah Garvey

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com